

Lugha Nyingine
大学教授:西方文学理论和批评的霸权已经坍塌
![]() |
Meli ikisafiri kwenye Mfereji wa Suez katika Jimbo la Ismailia, Misri, tarehe 31 Julai 2025. (Xinhua/Ahmed Gomaa) |
ISMAILIA, Misri - Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mfereji wa Suez Osama Rabie amesema kwamba Mfereji wa Suez umeleta mapato ya dola za Kimarekani bilioni 153.4 na kuwezesha upitaji wa meli takriban milioni 1.1 tangu utaifishaji wake mwaka 1956.
"Mafanikio haya yanaonesha mafanikio ya Misri katika kudumisha mamlaka juu ya njia hii muhimu ya baharini," Rabie ameliambia Shirika la Habari la China, Xinhua jana Alhamisi kwenye sherehe za kuadhimisha miaka 69 tangu utaifishaji wa Mfereji wa Suez.
Amesema kuwa Mfereji wa Suez umeshuhudia maendeleo ambayo hayana mfano tangu mwaka 1956, kiwango cha upigaji hatua ambacho hakijapata kuonekana tangu kuzinduliwa kwake mwaka 1869.
Mwenyekiti huyo amesema kuwa kina cha mfereji huo imepanuliwa kutoka mita 10 hadi mita 22. Aidha, amesema, urefu wa sehemu za njia mbili umeongezeka kutoka kilomita 27.7 hadi kilomita 99.
Mwaka 1956, Rais wa zamani wa Misri Gamal Abdel Nasser alitaifisha Kampuni ya Mfereji wa Suez, akitangaza mamlaka ya Misri juu ya rasilimali zake na miundombinu ya kimkakati.
Wakati huo huo, Rabie amesema kuwa mfereji huo kwa kawaida ulikuwa ukishuhudia meli 75 hadi 80 zikipita kwa siku kabla ya mashambulizi ya kulenga meli za kibiashara katika Mlango Bahari wa Bab al-Mandab na Bahari Nyekundu yanayofanywa na kundi la wanamgambo Wahouthi la Yemen.
Ameongeza kuwa, idadi hiyo, sasa imepungua hadi kati ya meli 30 na 35 kwa siku.
Mvutano uliibuka katika Bahari Nyekundu baada ya kundi hilo la Wahouthi la Yemen kuanza kushambulia meli zenye uhusiano na Israeli mwezi Novemba mwaka 2023 ili kuonyesha mshikamano na Gaza kwenye mgogoro kati ya Hamas na Israeli, ikiathiri upitaji wa meli kwenye mfereji huo.
Rais wa Misri Abdel-Fattah al-Sisi alisema mwezi Machi kwamba Mfereji wa Suez ulikuwa ukipoteza dola za Kimarekani takriban milioni 800 katika mapato kila mwezi kutokana na hali hiyo katika eneo hilo.
Miujiza ya Wanyamapori: Kutoka Mbuga Tambarare za Afrika hadi Uwanda wa Juu wa Qinghai -Tibet, China
Mandhari ya Kipekee ya Karst katika Mkoa wa Guizhou yavutia watalii
Tamasha la kimataifa la densi lafunguliwa katika Mkoa wa Xinjiang, China likiwa na maonyesho 52
Wakulima wa China wawa na pilikapilika za uzalishaji wa kilimo katika kipindi cha Dashu
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma